![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjy94HyrV-X7UCMm-zuF9vfh8WgjZxzAzf189y-hOwTEUoHc4SAYgSti_bIaNYxxZhzcdt0zcehalzozrczYDv_ILoXG_Wj3Iirxv3gVhiGxU4zhk65g3EbrbMv0Ub-0GlpLPY-WLCw25vP/s640/1.jpg)
Mgombea urais wa Tanzania kupitia Chama cha Chaumma, Hashimu Rungwe, ametangaza kuzindua kampeni zake za urais wa chama hicho Jumamosi tarehe 5 Septemba 2020 Manzese jijini Dar es Salaam.
“Chaumma itaongea na wananchi 5 Septemba 2020 katika Uwanja wa Manzese Dar es Salaam kuanzia saa 8 mchana. Wananchi waje wasikilize, tunachowaambia. Wakija pale watapata kila kitu na watauliza maswali na tutawajibu.Wako watu wenye hamu ya ubwabwa waje tutajua tunawapatiaje,” amesema Rungwe