Picha : EMMANUEL NTOBI, SALOME MAKAMBA WARUDISHA KWA KISHINDO FOMU KUGOMBEA UBUNGE SHINYANGA MJINI KUPITIA CHADEMA


Na Kadama Malunde – Malunde 1 blog
Wanachama wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Emmanuel Ntobi (aliyekuwa diwani wa Kata ya Ngokolo na Mwenyekiti CHADEMA mkoa wa Shinyanga) na Salome Makamba (aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalum) wamerudisha kwa kishindo Fomu za kuomba kugombea nafasi ya ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini leo Ijumaa Julai 10,2020.

Makada hao wa CHADEMA wamewasili katika Ofisi za CHADEMA Jimbo la Shinyanga Mjini wakisindikizwa na misafara ya wafuasi wa CHADEMA waliokuwa wanaendesha magari na pikipiki huku wakiwa wamebeba bendera za chama hicho sambamba na matarumbeta ya hapa na pale.

Mara baada ya kuwasili katika ofisi za CHADEMA Jimbo la Shinyanga Mjini, watia nao walikabidhi fomu za kuomba ridhaa ya kuchaguliwa na chama chao kugombea ubunge jimbo la Shinyanga Mjini kisha wakapata nafasi ya kuelezea mbele ya wanachama wa CHADEMA malengo yao ya kuomba chama kiwapitishe kuwania nafasi ya Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini.

Katibu wa CHADEMA Jimbo la Shinyanga Mjini Joseph Ndatala amesema zoezi la kurudisha fomu kwa wanachama wa CHADEMA waliotia nia kugombea ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini ni leo Ijumaa Julai 10 saa 10 kamili jioni.

“Zoezi linalofanyika leo ni kupokea fomu za wanachama wetu waliojitokeza kuomba kugombea nafasi ya Ubunge katika Jimbo la Shinyanga ambapo majina ya waliojitokeza yatajadiliwa katika mkutano wa chama na atapatikana mgombea mmoja”,amesema Ndatala.

Ameyataja majina ya wanachama wa CHADEMA waliochukua fomu kugombea ubunge katika Jimbo la Shinyanga Mjini kuwa ni Emmanuel Ntobi, Samson Ng’wagi, Mchungaji Jilala Fumbuka, Nicholaus Luhende, Hassan Salim pamoja na Zainab Kheri Zena Gulam wanaowania nafasi ya Ubunge Viti Maalum.

Ndatala amesema zoezi la wanachama wa CHADEMA kurudisha fomu za kugombea ubunge jimbo la Shinyanga Mjini limeenda sambamba na kumdhamini Tundu Lissu kuwa mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CHADEMA.

ANGALIA PICHA HAPA CHINI
Katibu wa CHADEMA Jimbo la Shinyanga Mjini Joseph Ndatala  akizungumza wakati wa kupokea fomu za wanachama wa CHADEMA waliojitokeza kuwania nafasi ya Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Katibu wa CHADEMA Jimbo la Shinyanga Mjini Joseph Ndatala  akizungumza wakati wa kupokea fomu za wanachama wa CHADEMA waliojitokeza kuwania nafasi ya Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini.
Katibu wa CHADEMA Jimbo la Shinyanga Mjini Joseph Ndatala  akipokea fomu ya Emmanuel Ntobi kuwania nafasi ya Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini.
Katibu wa CHADEMA Jimbo la Shinyanga Mjini Joseph Ndatala  akipokea fomu ya Emmanuel Ntobi kuwania nafasi ya Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini.
Katibu wa CHADEMA Jimbo la Shinyanga Mjini Joseph Ndatala  akionesha fomu ya Emmanuel Ntobi kuwania nafasi ya Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini.
Mtia nia kugombea ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini kupitia CHADEMA  Emmanuel Ntobi akieleza sababu zilizomsukuma kuomba chama chake kimpe ridhaa ya kugombea  Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini.
Mtia nia kugombea ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini kupitia CHADEMA  Emmanuel Ntobi akieleza sababu zilizomsukuma kuomba  chama chake kimpe ridhaa ya kugombea  Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini.
Mtia nia kugombea ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini kupitia CHADEMA  Emmanuel Ntobi akieleza sababu zilizomsukuma kuomba chama chake kimpe ridhaa ya kugombea  Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini.
Mtia nia kugombea ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini kupitia CHADEMA  Emmanuel Ntobi akieleza sababu zilizomsukuma kuomba chama chake kimpe ridhaa ya kugombea  Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini.
Katibu wa CHADEMA Jimbo la Shinyanga Mjini Joseph Ndatala  akipokea fomu ya Samson Ng'wagi kuwania nafasi ya Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini.
Katibu wa CHADEMA Jimbo la Shinyanga Mjini Joseph Ndatala  akipokea fomu ya Samson Ng'wagi kuwania nafasi ya Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini.
Mtia nia kugombea ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini kupitia CHADEMA  Samson Ng'wagi akieleza sababu zilizomsukuma kuomba chama chake kimpe ridhaa ya kugombea  Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini.
Mtia nia kugombea ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini kupitia CHADEMA  Salome Makamba akiwasili katika ofisi za CHADEMA Jimbo la Shinyanga Mjini kurudisha fomu ya  kuomba chama chake kimpe ridhaa ya kugombea  Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini.
Katibu wa CHADEMA Jimbo la Shinyanga Mjini Joseph Ndatala  akipokea fomu ya Salome Makamba kuwania nafasi ya Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini.
Katibu wa CHADEMA Jimbo la Shinyanga Mjini Joseph Ndatala  akipokea fomu ya Salome Makamba kuwania nafasi ya Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini.
Mtia nia kugombea ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini kupitia CHADEMA  Salome Makamba akieleza sababu zilizomsukuma kuomba chama chake kimpe ridhaa ya kugombea  Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini.
Mtia nia kugombea ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini kupitia CHADEMA  Salome Makamba akieleza sababu zilizomsukuma kuomba chama chake kimpe ridhaa ya kugombea  Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini.
Katibu wa CHADEMA Jimbo la Shinyanga Mjini Joseph Ndatala  akipokea fomu ya Zena Gulam kuwania nafasi ya Ubunge Viti Maalum Jimbo la Shinyanga Mjini.
Mtia nia kugombea ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini kupitia CHADEMA  Zena Gulam akieleza sababu zilizomsukuma kugombea  Ubunge Viti Maalum Jimbo la Shinyanga Mjini.
Awali Makada wa CHADEMA wakiendelea na shamra shamra nje ya ofisi za CHADEMA Jimbo la Shinyanga Mjini.
Awali Makada wa CHADEMA wakiendelea na shamra shamra nje ya ofisi za CHADEMA Jimbo la Shinyanga Mjini.
Msanii Mussa Jumanne akitoa burudani wakati makada wa CHADEMA wakirudisha  fomu kuomba kugombea ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini.
Msanii Mussa Jumanne akitoa burudani wakati makada wa CHADEMA wakirudisha  fomu kuomba kugombea ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini.
Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527