BODI YA MIKOPO ELIMU YA JUU YAFUNGUA DIRISHA LA MAOMBI KWA SIKU 40, YATOA MUONGOZO

Tunapenda kuwafahamisha wanafunzi wahitaji wanaotarajia kuomba mikopo ya elimu ya juu inayotolewa na Serikali kupitia HESLB kuwa mfumo wa uombaji wa mkopo kwa njia ya mtandao utakuwa wazi kwa siku 40 kuanzia Jumanne, Julai 21, 2020 hadi Jumatatu, Agosti 31, 2020.

Tunawashauri wanafunzi wahitaji kutumia muda wa sasa hadi mfumo utakapofunguliwa (Julai 16, 2020 hadi Julai 21, 2020) kusoma ‘Mwongozo wa Utoaji Mikopo kwa Mwaka 2020/2021’ unaopatikana kuanzia sasa katika tovuti ya HESLB (www.heslb.go.tz) katika lugha za Kiswahili na Kiingereza.

Mwongozo huu unatoa maelekezo ya kina kuhusu sifa, utaratibu na vigezo vitakavyotumika katika uchambuzi wa upangaji mikopo kwa mwaka wa masomo 2020/2021.

Aidha, baada ya kuusoma, tunasihi waombaji mikopo kuhakikisha wanaandaa nyaraka zote muhimu kama zinavyoelekezwa katika Mwongozo huo.

Imetolewa na:
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu
_________
1. Kupata Mwongozo kwa Kiswahili==> Bonyeza hapa

2.Guidelines and Criteria in English ==>Click here


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527