MWENYEKITI WA CHADEMA FREEMAN MBOWE AVAMIWA NA KUSHAMBULIWA



Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Taifa na Kiongozi wa Kambi ya Rasmi ya Upinzani Bungeni  Freeman Mbowe ameshambuliwa na kujeruhiwa na Watu wasiojulikana wakati akirejea nyumbani kwake jijini Dodoma usiku wa kuamkia leo Jumanne Juni 9,2020.


Msemaji wa CHADEMA Tumaini Makene amethibitisha kuwa Mbowe amevamiwa na kushambuliwa na watu wasiojulikana.



"Ni kweli ameshambuliwa na ameumizwa,amepelekwa Hospitali kwa ajili ya matibabu. Tutatoa taarifa zaidi baaadae",amesema Makene.



Taarifa zaidi zinakuja hivi punde...

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527