JAMII YATAKIWA KUWAFICHUA WAUZA DAWA ZA KULEVYA


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu ameitaka jamii mkoani Tanga kuibua na kuwafichua wauzaji na wasambazaji wa dawa za kulevya.

Waziri Ummy ametoa kauli hiyo jana wakati wa uzinduzi wa jengo la huduma za Methadone uliofanyika jijini Tanga.

Amesema jitihada zilizofanywa na serikali mara baada ya kuanzishwa kwa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) zimesaidia kuthibiti dawa hizo kwa asilimia 90.

Mpaka sasa serikali imezindua vituo nane vya methadone ambavyo ni Muhimbili, Temeke, Mwananyamala, Mwanza, Dodoma, Mbeya, Pwani na Tanga.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527