WANAFUNZI WA KIDATO CHA SITA KUANZA KUFANYA MTIHANI WAO WA MWISHO KESHO


Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Tanzania Dkt Charles Msonde

Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Tanzania Dkt Charles Msonde, amesema jumla ya watahiniwa 85,546 ndiyo waliosajiliwa kufanya mitihani ya kidato cha sita na ualimu inayotarajiwa kuanza nchi nzima hapo kesho Jumatatu Juni 29, 2020.

Msonde amesema maandalizi yote yameshakamilika na kupitia mtihani huo watahiniwa hao ndiyo watakuwa wanapimwa uelewa wao katika masomo waliyokuwa wakisoma.

Aidha baraza pia limezitaka kamati za mikoa za kusimamia mitihani kuhakikisha wanasimamia mitihani hiyo na kusitokee udanganyifu wowote kwa watahiniwa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527