RWANDA YAONGEZA SIKU 11 ZA WATU KUBAKI NYUMBANI ILI KUKABILIANA NA CORONA

Baraza la mawaziri nchini Rwanda limepitisha kuendelea kutekelezwa kwa amri ya kusitishwa shughuli za kawaida nchini humo siku zingine 11.

Hii inajiri wakati idadi ya watu walioambukizwa virusi vya Corona nchini humo ikifikia 143 , huku watu wengine 65 wakithibitishwa kupona.

Nchini Rwanda polisi wameanza kutumia ndege ndogo zisizo na rubani, kuwahamasisha watu mitaani kuheshimu amri ya kubakia nyumbani kama mkakati wa kuzuia kusambaa kwa virusi virusi vya Corona.

Hata hivyo hakuna kifo kinachohusiana na ugonjwa aw Covid-19 ambacho kimetokea nchini Rwanda


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post