CHINA YAIPA WHO DOLA MILIONI 50 BAADA YA MAREKANI KULIKATIA MISAADA SHIRIKA HILO


China inasema itatoa mchango wa Dola Milioni 30 kwa Shirika la Afya Duniani WHO, kulisaidia kupambana na maambukizi ya virusi vya Corona, ugonjwa unaosubua ulimwengu.

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya nje nchini humo Hua Chunying kupitia ukurasa wake wa Twitter amethibtisha hilo na kusema mchango huo unalenga kulisaidia shirika hilo kupambana virusi katika nchi zinazoendelea.

Aidha, amesema kuwa tayari China imetoa Dola Milioni 20, mchango uliotoa kwa WHO mwezi Machi.


Hatua hii ya China imekuja wiki moja baada ya rais wa Marekani Donald Trump kutangaza kuwa nchi yake inasitisha mchnago Wake kwa Shirika hilo kwa madai ya kushindwa kudhibiti mapema virusi hivyo.

Hatua hiyo ya Marekani  ilaaniwa na China na mataifa mengine ya Magharibi huku WHO ikisema huu sio wakati wa kusitisha mchango  huo wa fedha.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527