WAGONJWA WA CORONA NCHINI KENYA WAFIKA 50


Waziri wa Afya wa Serikali ya Kenya Mutahi Kagwe leo Jumatatu Machi 30 ametangaza wagonjwa nane zaidi wa ugonjwa wa virusi vya corona COVID-19 na kufanya idadi ya wagonjwa nchini humo kufikia 50.

Kwa mujibu wa gazeti la Daily Nation, waziri Kagwe amesema kuwa wagonjwa hao nane wameambukizwa virusi vya corona ndani ya nchi na kutoa tahadhari ya ugonjwa huo kuenea ndani kwa kuwa hakuna maambukizi mapya kutoka nje.

Mpaka Jumamosi Kenya ilikuwa na wagonjwa 38. Jana Jumapili waziri Kagwe alitangaza wagonjwa wapya wanne na kufanya idadi kufikia 42, hivyo idadi ya wagonjwa wapya 12 nchini humo imetangazwa ndani ya siku mbili tu.

Mtu mmoja tayari amepoteza maisha nchini humo kutokana na virusi hivyo.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527