TUME YA USHINDANI (FCC) YAONYA UPANDISHAJI BEI VIFAA VYA KUJIKINGA CORONA


Tume ya Ushindani (FCC) nchini Tanzania imewapa onyo waingizaji, wazalishaji, wasambazaji na wauzaji wa jumla na rejareja wa bidhaa za kujikinga na maambukizi ya virusi ya corona ikisema ni kinyume cha sheria ya ushindani.


Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa tume hiyo, jana Ijumaa Machi 19,2020 imesema kumekuwa na malalamiko ya wananchi kuhusu upatikanaji wa bidhaa hizo ambazo ni pamoja na dawa za kutakasa mikono na maeneo yanayoweza kuguswa kwa mikono (Hand Sanitizers), barakoa (face masks) na Vizuizi vya mikono (gloves).

“Baada ya Serikali kutangaza kuwa virusi vya corona vimeingia nchini na kutolewa kwa miongozo ya namna ya kujikinga na maambukizi, wananchi wamejitokeza kwa wingi kununua bidhaa za kujikinga dhidi ya maambukizi ya virusi hivyo.”

“Tume imepokea malalamiko juu ya uhaba na kuongezeka kwa kasi kwa bei za bidhaa hizo,” imesema sehemu ya taarifa ya tume hiyo.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post