Breaking : MGONJWA WA CORONA TANZANIA AFARIKI DUNIA

 Mgonjwa wa virusi vya corona nchini Tanzania amefariki dunia leo Jumanne Machi 31, 2020.

Taarifa iliyotolewa leo na Waziri wa Afya wa Tanzania, Ummy Mwalimu imethibitisha kifo hicho na kubainisha kuwa alikuwa akipatiwa matibabu katika kituo cha matibabu ya wagonjwa wa Covid-19 kilichopo Mloganzila.

"Marehemu ni Mtanzania mwanaume mwenye umri wa miaka 49 ambaye pia alikuwa akisumbuliwa na maradhi mengine.Tunamuomba Mungu ailaze roho yake mahala pema peponi, na tunatoa pole kwa familia, ndugu jamaa wa marehemu, " amesema Ummy.




Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527