VIFO VYA BARABARANI VYAPUNGUA TANGA


Mkuu wa kikosi cha usalama barabara mkoa wa Tanga Solomon Mwangamilo akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi wa usalama barabara kwa shule za msingi na sekondari Jijini Tanga
MKURUGENZI wa Jiji la Tanga Daudi Mayeji akizungumza wakati wa uzinduzi huo
MWAKILISHI wa Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Abdurahaman Shiloo ambaye ni Diwani wa Kata ya Mzingani na Mwenyekiti wa Kamati ya Elimu,Afya na Mazingira akizungumza wakati wa halfa hiyo
Mkurugenzi wa Asasi inayojishughulisha na Usalama Barabara ya Amend Tom Bishop akizungumza wakati wa halfa hiyo


 MWAKILISHI wa Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Abdurahaman Shiloo ambaye ni Diwani wa Kata ya Mzingani na Mwenyekiti wa Kamati ya Elimu,Afya na Mazingira wa pili kutoka kushoto akikata utepe wakati wa uzinduzi huo


 MWAKILISHI wa Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Abdurahaman Shiloo ambaye ni Diwani wa Kata ya Mzingani na Mwenyekiti wa Kamati ya Elimu,Afya na Mazingira wa pili kutoka kushoto akikata utepe wakati wa uzinduzi huo

 MEZA Kuu wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa uzinduzi huo
 SEHEMU ya wanafunzi wa shule za Msingi Chuma, Masiwani,Kana na Shule ya Sekondari Maawal
MKURUGENZI wa Jiji la Tanga Daudi Mayeji  kushoto akiwa na Mwakilishi wa Meya wa Jiji la Tanga Abdurahaman Shiloo akiwa na Mkuu wa kikosi cha usalama barabara mkoa wa Tanga Solomon Mwangamilo wakati wa uzinduzi wa mradi wa usalama barabara kwa shule za msingi na sekondari Jijini Tanga.
 Wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya uzinduzi huo

Udhibiti wa makosa ya usalama barabara mkoani Tanga umesaidia kupunguza matukio ya ajali zilizohusisha watoto kutoka 41mwaka 2018 hadi kufikia ajali 9mwaka 2019.

Takwimu hizo zimetokewa na Mkuu wa kikosi cha usalama barabara mkoa wa Tanga Solomon Mwangamilo wakati wa uzinduzi wa mradi wa usalama barabara kwa shule za msingi na sekondari Jijini Tanga.

Alisema kuwa ukaguzi wa Mara kwamara ya vyombo vya moto pamoja na elimu ya usalama barabara ndio imeweza kusaidia kupunguza ajali hizo.

"Changamoto pekee iliyobaki kwa  Sasa ni watoto chini ya miaka 9  kupakiwa kwenye usafiri wa bodaboda zaidi ya watatu kwa ajili ya kupelekwa shule Jambo ambalo ni hatari kwa usalama wao "alisema RTOMwangamilo.

Aidha alisema kuwa kupitia mradi huo anaamini utaweza kuja na suluhisho la kumaliza ajali za barabara kwa wanafunzi hususani katika shule ambazo zipo karibu na maeneo yabarabara kuu.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa asasi inayojishughulisha na usalama barabara  Amend Tom Bishop alisema kuwa mradi huo utasaidia kujenga vivuko katika maeneo ya shule pamoja na kutoa elimu ya matumizi ya barabara kwa wanafunzi.

"Tunajua kwamba maendeleo ya miji mikubwa duniani inakuja na changamoto ya ongezeko la ajali hivyo kupitia mradi huu tumekuja kusaidiana na serikali katika kuhakikisha ndoto ya mtoto wa kitanzania inatimia"alisema Bishop

Nae Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Daudi Mayeji alisema kuwa mradi kupunguza ajali ambazo walikuwa wanapata wakati wanapokwwnda shule na wanaporudi nyumbani.

"Sasa Kuna njia maalum ya kupitia waenda kwa miguu kwani awali vyombo vya moto na watembea kwa miguu walikuwa wanatumia kwa pamoja na hivyo kuweka hatari ya uwepo wa ajali"alisema Mayeji

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527