ALIYEKUWA KATIBU MKUU CHADEMA DR. VICENT MASHINJI ATAMBULISHWA RASMI CCM

Viongozi waandamizi watano kutoka vyama vya upinzani wametambulishwa  leo na kupokelewa rasmi kuwa wana CCM mbele ya Mwenyekiti wa Chama hicho Rais John Pombe Magufuli na wajumbe wa Kikao cha Kamati Kuu kilichofanyika Ofisi Ndogo ya CCM mtaa wa Lumumba jijini Dar es salaam.



Kutoka kushoto ni aliyekuwa Katibu Mkuu wa CHADEMA Dkt. Vincent Mashinji, aliyekuwa Meya wa jiji la Arusha kupitia CHADEMA Bw. Kalisti Lazaro,  aliyekuwa Meya wa Jiji la Mbeya kupitia tiketi ya CHADEMA Mchungaji David Mwashilindi .


Wengine ni aliyekuwa Mbunge wa Tandahimba kupitia CUF, Bw. Katani Ahmed Katani na aliyekuwa Naibu Meya wa Jiji la Mbeya kupitia tiketi ya CHADEMA Bw. Fanuel Kyanula



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527