MWENYEKITI WA CHADEMA JIMBO LA BUNDA AJIUNGA NA CCM LEO


Diwani kutoka Kata ya Hunyari iliyopo Halmashauri ya Bunda mkoani Mara Makina Josephat ametangaza kuhama Chadema na kuhamia CCM.

Makina ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chadema Jimbo la Bunda na Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama hiko kikuu cha upinzani ametangaza uamuzi wake huo leo jijini Dodoma na kupokelewa na MNEC wa CCM, Ismail Jamaa.

Akizungumza baada ya kumpokea Diwani huyo, MNEC Jamaa amesema wamempokea kiongozi huyo kwa niaba ya Katibu Mkuu wa CCM Taifa na kwamba taratibu zingine za kumpokea zitafanyika wilayani Bunda ambapo anaishi.

Nae Makina amesema kwa miaka minne ambayo Rais Dk John Magufuli ameongoza amegusa kila sekta na kumaliza ajenda zote ambazo wapinzani walikua wakizipigania hivyo haoni haja tena ya kuendelea kuwepo upinzani.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527