KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA SHERIA NDOGO KUSIKILIZA MAONI YA WADAU JAN, 31 ,2020

Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Sheria ndogo imepanga  kufanya mkutano  wa kusikiliza Maoni ya wadau [Public Hearing ]kuhusu Muswada wa sheria wa usuluhishi ya Mwaka  2020[The Arbitration Bill 2020] kwa mujibu ya kanuni  ya 84[2] ya kanuni za kudumu za Bunge,Toleo la Januari ,2016,ambapo Muswaada huo umesomwa  kwa mara ya kwanza   Bungeni tarehe 28,Januari,2020.


Katika taarifa iliyotolewa na kitengo cha Mawasiliano  na Uhusiano wa kimataifa  ofisi ya Bunge Januari 28,2020  jijini Dodoma imefafanua kuwa mkutano huo wa kusikiliza maoni ya wadau[Public Hearing ]utafanyika siku ya Ijumaa  tarehe 31,Januari,2020 saa saba mchana  katika ukumbi Na. 229 jengo la Utawala Bungeni jijini Dodoma.

Aidha,katika taarifa ya kitengo hicho cha Mawasiliano na Uhusiano wa kimataifa Ofisi ya Bunge imeendelea kufafanua kuwa ,kwa kuzingatia umuhimu wa muswada huo ,kamati inawaalika wadau wote  kufika na kuwasilisha maoni  ya wadau ambapo pia Maoni ya wadau yanaweza kuwasilishwa   kwa barua pepe cna@bunge.go.tz  na muswada  unaweza kupakuliwa kupitia   www.parliament.go.tz.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527