YANGA YATANGAZA KATIBU MKUU MPYA


Makao makuu ya Yanga mitaa ya Jangwani Dar es salaam.

Klabu ya soka ya Yanga Novemba 11, 2019, imetangaza uteuzi wa Katibu Mkuu mpya, ambaye anakuwa mtendaji mkuu wa klabu hiyo.

Taarifa ya Yanga imemtaja David M. Ruhago kuwa ndio Katibu Mkuu, ambaye ameteuliwa na Kamati ya Utendaji ya klabu hiyo chini ya Mwenyekiti wake Dkt. Mshindo Msolla.

Aidha taarifa hiyo imeeleza kuwa uteuzi huo unaongeza idadi ya watendaji ndani ya klabu hiyo.

Ruhago amekuwa mjumbe wa kamati mbalimbali za klabu hiyo katika vipindi tofauti tofauti.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527