CHAMA CHA ADC CHATANGAZA KUSHIRI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA

Chama cha Alliance for Democratic Change (ADC) kimesema licha ya baadhi ya wagombea wake kuenguliwa katika uchaguzi wa serikali za mitaa, kitashiriki uchaguzi huo utakaofanyika Novemba 24, 2019.



Katibu mkuu wa chama cha ADC, Hassan Doyo amezungumza na waandishi wa habari leo kwenye makao makuu ya chama hicho na kuweka wazi kuwa hawatajitoa kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa ambao unatarajiwa kufanyika Novemba 24, 2019.

Wakati ADC wakieleza hayo vyama vya Chadema, NCCR-Mageuzi, UPDP, NLD, Chauma, ACT-Wazalendo na CUF vimeshatangaza kutoshiriki uchaguzi huo kwa madai ya kutotendewa haki ikiwa ni pamoja na wagombea wake wengi kuenguliwa.

“Sisi ni mabingwa wa changamoto hatupelekwi na mihemko ya watu, tunapelekwa na misingi ya chama cha siasa kwa sababu hata walipofuta matokeo ya uchaguzi Zanzibar wengine walisusa lakini sisi hatukufanya hivyo,” amesema Doyo


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527