WAANDISHI WA HABARI MWANZA WAKUMBUSHWA WAJIBU WAO KUELEKEA UCHAGUZI

Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa Mwanza (MPC) kwa kushirikiana na Taasisi ya Mwalimu Nyerere (MNF), imetoa mafunzo kwa waandishi wa habari mkoani Mwanza kwa lengo la kuwajengea uwezo kuripoti kwa weledi habari kuhusu ujenzi wa amani kabla, wakati na baada ya uchaguzi. Mafunzo hayo yamefanyika Oktoba 31, 2019 Holmand Hotel jijini Mwanza.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
 Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa Mwanza (MPC), Edwin Soko akitoa salamu kwenye ufunguzi wa warsha hiyo.
 Mratibu wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa Mwanza (MPC), Rose Mwanga akitoa neno la shukurani wakati wa kuahirisha mafunzo hayo.
Wanahabari wakimsikiliza na kunasa habari kwenye warsha hiyo. 
 Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo yenye Tija kwa Watu wote (PCD), Prof. Francis Matambalya akitoa utambulisho kuhusu Taasisi ya Mwalimu Nyerere (MNF) kwenye warsha hiyo. PCD ni idara ndani ya MNF.
 Mafunzo hayo yalilenga kuwajengea uwezo wanahabari mkoani Mwanza kuandika habari kwa weledi kabla, wakati na baada ya chaguzi.
Tazama Video hapa chini


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527