RAIS MAGUFULI KUTUNUKIWA SHAHADA YA HESHIMA YA UDAKTARI WA FALSAFA NA CHUO KIKUU CHA DODOMA KESHO


Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) kesho kitamtunukia Rais Dk. John Magufuli Shahada ya Heshima ya Daktari wa Falsafa (Honorary PhD) kwa uongozi wake hususani katika ujenzi wa uchumi wa viwanda, kuwekeza kwenye elimu, miundombinu, kuimarisha utawala bora, na mapambano dhidi ya rushwa.

Akizungumza leo Jumatano Novemba 20, 2019 makamu mkuu wa chuo hicho, Profesa Faustine Bee amesema shahada hiyo itatolewa kesho katika mahafali ya 10 ya chuo hicho.

Profesa Bee amesema wahitimu 6,488 watatunukiwa astashahada, shahada, stashahada ya juu, shahada ya umahiri, na shahada ya uzamivu.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527