CHADEMA WALIMWA BARUA NA MSAJILI WA VYAMA KWA KUTOFANYA UCHAGUZI WA VIONGOZI WA JUU WA CHAMA......WAPEWA SIKU 7 ZA KUJIELEZA


Msajili wa Vyama vya Siasa nchini Tanzania ameandika barua kwenda kwa chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema akikitaka kutoa maelezo kwa nini kisichukuliwe hatua kwa kutokufanya uchaguzi wa viongozi wake.

Barua ya Msajili iliyoandikwa Oktoba 1, 2019 na kusainiwa na Sisty Nyahonza kwa niaba ya msajili wa vyama vya siasa inasema uongozi wa Chadema chini ya Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe umemaliza muda wake tangu Septemba 14, 2019.

Katika barua hiyo, msajili amekitaka chama hicho kutoa maelezo hayo kabla ya Oktoba 7, 2019 saa 9:30 mchana.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527