IGP SIRRO AWAUMBUA MAKAMANDA WA POLISI WANAOONESHA WATUHUMIWA HADHARANI ....."UNATAFUTA SIFA?"


Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Simon Sirro jana alitumia takribani dakika 70 kukemea, kuonya na kutoa mwongozo, akitaka maofisa wa chombo hicho wafuate dira yake kwa kuwa anayeweza kushika cheo alichonacho ni “mtu mmoja tu” na muda wake ukifika ataondoka.


Hotuba hiyo ya Kamanda Sirro pia iligusia maofisa ambao wamekuwa wakiwahukumu watuhumiwa katika mikutano na waandishi wa habari.

“Huwa nashangaa. Wakati mwingine hivi unamchukua mtuhumiwa, unamuweka pale unamuonyesha kila wakati. Unatafuta sifa?” alihoji.

“Hivi kwenye upelelezi katika mazingira ya kawaida huyo si mtuhumiwa tu? Leo unamtoa hadharani kaiba, unasahau kesho na keshokutwa. Kwenu huko Musoma anakushtaki kwamba kuna siku ulinidhalilisha mimi kuwa mwizi. Vitu vingine tushauriane, si ndiyo.”

Mmoja wa maofisa ambao wamekuwa wakitangaza hadharani watuhumiwa ni kamanda wa Dodoma, Gilles Muroto ambaye huwaonyesha watuhumiwa mbele ya waandishi, kutaja uhalifu anaodai wamefanya na baadaye kusema walikiri katika mahojiano na polisi.
TAZAMA VIDEO <<HAPA>>

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527