WAANDISHI WA HABARI WATAMBULISHA KUNDI LA 'STRONG DADAZ JOURNALIST' ...DC MAHUNDI ATIA NENO



Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mkoani Mbeya,Mhandisi MaryPrisa Mahundi akiwa katika picha ya pamoja na kikundi cha Strong Dadaz Journalist

Na Esther Macha,Chunya
Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mkoani Mbeya,Mhandisi MaryPrisa Mahundi amewataka wanawake kuendelea kujituma kufanya kazi ili kuongeza thamani yao katika maisha badala ya kutegemea kuolewa.

Akizungumza  na waandishi wa habari wanawake waliomtembelea ofisini kwake kwa lengo la kutambulisha kikundi chao kinachojulikana Strong Dadaz Journalist kilichopo Mkoani Mbeya.

Mhandisi Mahundi aliwataka wanapofanya kazi pia kazi wajitahidi kumtanguliza mungu wakati wanafanya kazi zao za kila siku ili waweze kufanikiwa katika shughuli zao.

Hata hivyo Mkuu huyo wa Wilaya alisema kuwa pia wajiongozee dhamani pamoja na kusaidiana wenyewe kwa wenyewe ili kufikia malengo waliyojiwekea ikiwa ni pamoja na kupendana.

“Siri ya Mwanamke ni kujishughulisha katika maisha msikate tama wanawake wenzangu kitendo cha nyie kuamua kuwa na umoja wenu ni faraja tosha kwenu”alisema Mkuu huyo wa Wilaya.

Aidha Mhandisi Mahundi alitoa kiasi cha shilingi laki tano kwa ajili ya kusaidia kikundi hicho cha Strong Dadaz Journalist ili kiweze kusajili Online Tv ambayo kikundi hicho kimedhamiria kufungua ili kuboresha huduma za kihabari kwa wanawake katika kurahisisha upatikanaji wa habari kwa wananchi.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Bomba Fm Radio ,Fredy Herbert aliahidi kuchangia kikundi hicho sh.100,000/= katika kusaidia kukamilisha usajili wa Online tv.

“Mhe. mimi nitakuwa na waandishi hawa pindi watakapohitaji msaada wa jambo lolote nitakuwa nao karibu katika kuwasaidia ",alisema Mkurugenzi huyo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527