SHEIKH TWAHILI ISMAIL TABILANE AREJEA KUTOKA MAKKA KUHIJI...AFANYIWA HAFLA YA MAPOKEZI MISENYI


Na Lydia Lugakila - Malunde1 blog 
Sheikh Twahili Ismail Tabilane (70)  mkazi wa kijiji cha Burembo kata ya Mushasha wilayani Misenyi mkoani Kagera amerejea salama hapa nchini akitokea Mji wa Makka Saudi Arabia katika kutekeleza ibada ya Hija ya dini ya kiislamu.


Akizungumza kwenye hafla ya kupongezwa kutoka katika ibada ya Hijja iliyofanyika Septemba 2, 2019, nyumbani kwake Burembo, Sheikh Ismail ambaye kwa sasa ni Khaji amesema kutokana na Umoja uliopo Makka ikiwemo ushirikiano na upendo ni ishara kuwa kila Muislamu aige na kujifunza.

Ameitaja safari hiyo kuwa  ni ya neema kubwa iliyosababisha yeye kurudi hapa nchini akiwa salama hivyo ametamani tena kurudi nchini makka.

Shekhe huyo amesema kila Muislamu aione habari ya kwenda hija kama ya kawaida na kuwa kila muumini wa dini hiyo atekeleze suala la kufika makka

"Namshukuru Mungu hali niliyoikuta kule Makka ni nzuri natamani kurudi mwaka ujao, hii ni neema kule hakuna cha tajiri wala maskini kule ni haki sawa kwa wote", amesema.

Amesema safari ya kwenda Hija haina ubaguzi kwani hija hiyo inawapa Waislamu wote haki sawa, ikiwemo chakula cha bure, malazi na mahitaji mengineyo muhimu pamoja na kupewa mafunzo ikiwemo kusoma vitabu vya Quran Tukufu vyenye maudhui ya kuiheshimu dini hiyo.

Kwa upande wake Sheikh Mkuu wa mkoa wa Kagera, Haruna Kichwabuta amewahimiza waislamu mkoani Kagera kuendelea kuwa wamoja na kumuomba Mungu ili kila muumini wa dini hiyo aweze kufikia Makka

Hata hivyo Sheikh Kichwabuta ameyashukuru madhehebu tofauti mkoani Kagera yaliyoshiriki kwa kumpokea Sheikh Twail aliyekwenda kuwakilisha dhehebu hilo katika ibada hiyo.

Amewataka Waislamu kujitokeza kwa wingi mwaka ujao 2020 kuudhuria ibada ya Hija. 

Naye Sheikh Mkuu Wilaya ya Misenyi mkoani, Abduzaydi Kyagulani ametoa pongezi kwa shekhe huyo kurejea salama hapa nchini na kuhimiza umoja kwa waumini hao na madhehebu tofauti ikiwemo kuiombea nchi amani 

Amesema Masheikh kutoka Kanyigo,Buyango, Kilimilile, Mtukula,Bugandika , Burembo wote wamerejea kwa usalama bila matatizo ambapo ameongeza kuwa madhumuni mazito ni kujenga nguzo tano za kiislamu sambamba na umoja.

Shekhe wa mkoa wa Kagera Haruna Kichwabuta akimpongeza Shekhe Ismail kwa kurejea kutoka Makka. Picha zote na 
Lydia Lugakila - Malunde1 blog 

Kushoto ni Sheikh Twahili Ismail Tabilane (70)  mkazi wa kijiji cha Burembo kata ya Mushasha wilayani Misenyi mkoani Kagera akizungumza baada ya kurejea kutoka Makka.

Shekhe wa mkoa wa Kagera Haruna Kichwabuta akizungumza wakati wa kumpokea 
Sheikh Twahili Ismail Tabilane  akitokea Makka.

Shekhe wa wilaya ya Misenyi mkoani Kagera Abduzayid Kyagulani akizungumza 
wakati wa kumpokea Sheikh Twahili Ismail Tabilane  akitokea Makka.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527