OFISI YA MAKAMU WA RAIS YAWAPA MAFUNZO KAMATI YA BUNGE


Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. George Simbachawene amesema mchakato wa Mkataba Minataka kuhusu Zebaki unaenda hatua kwa hatua ili kuwaandaa watu kuweza kupokea mabadiliko.

Mhe. Simbachawene amesema hayo jana Septemba mosi, 2019 wakati wa semina kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira ya Mkataba wa Minamata kuhusu Zebaki na Uwajibikaji kisheria na fidia kwa madhara yanayoweza kutokea kutokana na matumizi ya bioteknolojia iliyofanyika Jijini Dodoma.

Alisema Serikali iliridhia Mkataba wa Minamata ili kulinda afya ya binadamu na mazingira dhidi ya madhara yanayotokana na uchafuzi wa mazingira unaotokana na Zebaki. 

"Umoja wa Mataifa ulikaa na kuona kwa fundisho lililotokea Minamata huko Japan hivyo madhara hayo yasiendelee kutokea duniani pamoja na hayo lakini bado zebaki ina kazi ya kufanya unapotaka kuwatoa watu kutoka utamaduni mwingine mabadiliko yanakuwepo. 

"Pengine mnaweza kusema kwanini zebaki isipigwe marufuku mara moja mambo yanayobadilika yanafanywa polepole si kwa haraka na hatimaye watu wataelewa tu," alisema.

Awali aakiwasilisha mada hiyo, Mhandisi wa Viwanda kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais ambayo imeandaa semina hiyo Julius Enock alisema madhara yanayotokana na zebaki ni kuathiri mfumo wa neva za fahamu.

Katika kuathiri kwa mfumo huko inasababisha kusikia, kuongea, kuona, kumeng’enya, kumeza chakula, kutembea kuathiriwa pamoja na ukakamavu wa mwili. 

Aidha madhara mengine aliyotaja Enock ni kuathiri viungo muhimu vya mwili ambayo ni moyo, mapafu, ini, figo na hata mimba.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527