MSHAURI WA USALAMA WA TAIFA WA MAREKANI JOHN BOLTON AJIUZULU


Rais Donald Trump wa Marekani amesema mshauri wa usalama wa taifa wa Marekani John Bolton amejiuzulu baada ya kumuomba afanye hivyo. 

Trump alimtaka Bolton ajiuzulu Jumatatu jioni na kupokea barua ya kujiuzulu Jumanne asubuhi. 

Amesema kwenye ukurasa wake wa Twitter kuwa yeye na viongozi wengine hawakukubali mapendekezo yake mengi. 

Msemaji wa Ikulu ya Marekani Hogan Gidley aliwaambia wanahabari kuwa Trump na Bolton hawaelewani katika masuala mengi.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527