OPARESHENI YA KIJANI YATUA KIGOMA..... WAZEE WATAKIWA KUACHA KUTISHA VIJANA...WAPISHE NAFASI ZA UONGOZI

Na Rhoda Ezekiel - Kigoma
Wazee wametakiwa kutoa nafasi kwa vijana waweze kugombea katika nafasi za uongozi na kuacha tabia ya kuwatisha na kuwazuia vijana ili kuwajengea msingi mzuri na kuwapima katika nafasi mbalimbali ili kujenga viongozi watakaoongoza kwa hekima na busara.

Rai hiyo ilitolewa jana na Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi taifa (UVCCM) Kheri James  mkoani Kigoma wakati wa uzinduzi wa  'Oparesheni ya Kigoma ya Kijani'.

James alisema nchi inahitaji utayari wa vijana na uongozi wa vijana hivyo lazima wazeee wawaachie vijana kugombea na wasiwanyime nafasi ili waweze kuwapima na kuwajengea weledi wa uongozi na busara kwa kipindi hiki ambacho bado kuna wazee wenye busara ili waweze kuwapa busara hizo na waweze kubaki viongozi wazuri.

Alisema vijana wakipewa nafasi kwa kipindi hiki ambacho bado kuna wazee wa kuwapima kutokana na busara zao namna gani ya kuongoza, itasaidia kutengeneza taifa lenye uongozi ulio bora na unaozingatia misingi ya waasisi wa Taifa la Tanzania na kuepuka kuacha taifa la watu wanaofanya maamuzi bila kutumia busara.

Aidha James aliwataka wananchi wa mkoa wa Kigoma kuwapuuza wanasiasa wanaotumiwa na watu wa nje kuivuruga nchi, kwa kusema kwamb Tanzania kuna matatizo na hakuna kilichofanyika jambo ambalo sio kweli kwa kuwa mambo yaliyofanywa na Serikali iliyopo madarakani yanaonekana.

Alisema Siasa hazifai kutweza juhudi zinazofanywa na serikali kwa maslahi ya Taifa letu,  hivyo wanasiasa wanatakiwa kujua kazi yao ni kukosoa pale jambo linapoonekana haliendi sawa na kupongeza pale serikali inapofanya vizuri na sio kutumiwa na watu wa nje kuwakatisha tamaa viongozi wanaoifanya nchi isonge mbele kwa kuwa uchumi. 

Kwa Upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kigoma, Amandus Nzamba alisema watajitahidi kutoa  nafasi kwa vijana,  ili na wao waweze kujifunza namna ya kuongoza  na kuiletea nchi maendeleo.

Aidha aliwaomba vijana kujitokeza kwa wingi kugombea uongozi kuanzia ngazi ya serikali za mitaa hadi uongozi wa juu, kwa kuwa vijana wengi wanaogopa kujitokeza kugombea nafasi mbali mbali  hivyo sasa ni wakati wao.

Nae katibu wa Umoja wa Vijana(UVCCM) Kigoma Rashidi  Semindu alisema Vijana Kigoma wamejipanga katika chaguzi zinazokuja ikiwa ni pamoja na kulirudisha jimbo la kigoma mjini kwa chama cha mapinduzi na kuhakikisha vijana wote  wanajitokeza na kupambana na upinzani kwa Mkoa wa Kigoma.

Alisema wamefanikiwa kuwarudisha kwenye Chama Cha Mapinduzi vijana 82 wakiwemo waliokuwa Viongozi wa chama cha ACT wazalendo, wataendelea kuwashawishi vijana kutokana na mambo Makubwa yanayofanywa na viongozi wa CCM Kwa kuleta maendeleo Tanzania.

Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana (UVCCM)Taifa Kheri James pembeni ni Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Kigoma Silvia Sigula  akikaribishwa Mkoani Kigoma.

Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana (UVCCM)Taifa Kheri James pembeni ni Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Kigoma Silvia Sigula  akikaribishwa Mkoani Kigoma.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527