TANZANIA YAJIANDAA KUPOKEA UGENI WA KUTOKA JUMUIYA YA NCHI WANACHAMA KUSINI MWA AFRIKA (SADC)


Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara  Profesa Joseph Buchweishaija amewataka watanzania wote kujitokeza kwa wingi kushiriki katika maadhimisho na maonyesho ya nne ya wiki ya Viwanda ya Jumuia ya Maendeleo ya Kusini mwa Africa (SADC) . 



Maadhimisho na Maonesho hayo yatafanyika kuanzia tarehe 5 hadi 8 Agosti 2019 katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC); Viwanja vya Karimjee na Gymkhana jijini Dar es Salaam.

Profesa Bucheishaija amesema kuwa Serikali kupitia Wizara ya Viwanda na Biashara inawaalika wananchi kufika kwa wingi kwani tunatarajia jumla ya nchi  15 wanachama wa SADC zitashiriki,

Aidha, ameongeza kuwa wiki hii ya SADC itawawezesha wananchi kuona fursa mbalimbali ikiwemo kuweza kupata malighafi za kilimo ambazo viwanda utumia kuzalisha bidhaa za viwandani. Miongoni mwa faida watakazozipata watanzania kupitia maonesho ya Viwanda kwa nchi za Kusini mwa Afrika  ni pamoja na kujifunza au kubadilishana uzoefu na nchi nyingine za SADC ambazo zitashiriki katika maonesho hayo pamoja na kuongeza wigo wa masoko ya ndani na nje ya nchi.  



Nafasi imetolewa kwa kila mtanzania kujisajiri bado ipo mpaka tarehe 2 August, 2019 na wale ambao watakuwa hawajajisajiri  wasiwe na wasiwasi maana nao watatembelea maeneo ya maonesho kama wengine na kuweza kuona bidhaa za nchi nyinyine, hivyo watu wote wanakaribishwa sana kwa ajili ya tukio la kihistoria ambalo kutokea tena mpaka ipite miaka kumi na mitano. 



Naye Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda  na Biashara  ndugu Ludovick Nduhiye ametoa ufafanuzi kuwa lengo kuu ni kuweka utayari kwa wananchi hususani kwa Tanzania  kuweza kushiriki kwa wingi na kuweza kujionea fursa lukuki ambazo zitaonekana katika maoshesho hayo.  


Aidha bwana Nduhiye amewakaribisha wananchi kufika kwa wingi lengo likiwa ni   kuangailia fursa muhimu zitakazopatikana kwenye wiki hiyo ya viwanda ikiwa ni pamoja na upatikanaji wa masoko pamoja na ubadilishaji wa mawazo namna ya kuanzisha viwanda mbalimbali pamoja na kupata fursa mbalimbali kwenye nchi hizo za SADC. 


 Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya maonesho na maadhimisho ya Wiki ya Viwanda kupitia Wizara ya Viwanda na Biashara bwana Ally Gugu ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Mtengamano na Biashara amewahimiza wananchi kujisajili kupitia anuani zinazopatikana katika tovuti ya Wizara ya Viwanda na Biashara ambayo ni www.mit.go.tz na kisha kubofya katika  linki mbili za  haraka (quick link) ambazo ni Usajili Wiki ya Viwanda na Usajili Mkutano wa 39 wa SADC. 


Gugu aliongezea kuwa haya maonesho ya viwanda ni  fursa ya watanzania wote kuanzia wajasiriamali wadogo, wajasiriamali wa kati pamoja na wenye viwanda vikubwa ili tuweze kutimiza azima ya Serikali ya awamu ya tano inayosisitiza maendeleo kupitia uchumi wa Viwanda  ili Tanzania iweze kufikia uchumi wa kati.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post