MSD YAKABIDHI MADAWA MKOANI MOROGORO KWA AJILI YA MAJERUHI WA AJALI YA MOTO WA LORI LA MAFUTA


Mkurugenzi Mkuu wa MSD Laurean Bwanakunu akiwa pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Huduma kwa Wateja na Shughuli za Kanda wa MSD Salome Mallamia na Meneja wa MSD Kanda ya Dar es Salaam inayohudumia mkoa wa Morogoro Celestine Haule wakiendelea kupokea dawa zaidi za kukabidhi hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Morogoro kwa ajili ya kuhudumia majeruhi

…………………………………………………

Timu ya MSD ikiongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa MSD Bw. Laurean Bwanakunu wakiwa sambamba na Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Mohamed Kambi, wamewatembelea majeruhi wa ajali ya moto, iliyosababishwa na mlipuko wa lori la mafuta waliolazwa katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro.

Pamoja na kuwajulia hali majeruhi hao, ujumbe huo pia umelenga kufuatilia na kufahamu misaada ya haraka ya kitabibu inayohitajika kwa sasa hospitalini hapo ili kusaidia majeruhi.

Aidha, wajumbe hao, wamewasilisha msaada wa dawa na vifaa tiba kwenye hospitali hiyo.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527