MAWAKILI WATANO KUTETEA UBUNGE WA TUNDU LISSU MAHAKAMANI


Mawakili wanne wakiongozwa na Wakili Peter Kibatala watamtetea Tundu Lissu katika kesi ya kupinga kuvuliwa ubunge. Lissu anaiomba mahakama ibatilishe yeye kuvuliwa ubunge, izuie Mbunge Mteule, Miraji Mtaturu kuapishwa, na kuamuru Bunge kumlipa stahiki zake zote wakati akitibiwa.

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Alute Mughwai ambaye ni kaka yake Lissu amesema kesi hiyo itaanza kuunguruma Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam.

Mbali na Kibatala, mawakili wengine ni Jeremia Mbesya, John Malya na Fredi Kalonga.

Amebainisha kuwa maombi ya kufunguliwa kesi hiyo  chini ya hati ya dharura, kupitia kwake (Mughwai) aliyempa mamlaka ya kisheria kufanya hivyo, yatasikilizwa Agosti 21, 2019.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527