UPANDAJI HOLELA WA MITI KATIKA NJIA ZA UMEME KAHAMA WATAJWA KUSABABISHA NISHATI YA UMEME KUKATIKA

NA SALVATORI NTANDU

Upandaji holela wa miti katika njia kuu za Umeme Wilayani kahama mkoani Shinyanga umetajwa kuchangia kusababisha Nishati hiyo kukatika mara kwa mara kutoka na miti hiyo kugusa nyanya za Umeme.

Kauli hiyo imetolewa na Meneja wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) wilayani Kahama Mhandisi King Fokanya wakati akizungumza na waandishii wa habari ofini kwake kuhusiana namna walivyojipanga kutoa elimu kwa wananchi juu ya utunzaji wa miundombinu ya umeme.

Amesema katika maeneo mengi wilayani humu wananchi wamepanda miti mikubwa katika karibu na nguzo za umeme jambo ambalo linaweza kuleta madhara makubwa pindi nguzo zinapo anguka ama kuguswa na miti hiyo.

Amefafanua kuwa pindi Shirika hilo linapotaka kuikata baadhi yao wamekuwa wakilaumu juu ya ukataji wa miti hiyo katika njia za umeme na watumishi wake katika oparesheni za kuhakikisha miundombinu hiyo inakuwa salama.

Katika Hatua nyingine Mhandisi Fokanya amesema katika mwaka wa fedha wa 2019/2020 Ofisi yake imepokea shilingi milioni 847 kwa ajili ya kupeleka huduma ya nishati ya umeme kwenye kata 10 ambazo hazina umeme zilizopo Halmashauri ya Mji wa Kahama na Msalala.

Amefafanua kuwa  shilingi Milioni 847 zimegawanya katika makundi mawili ambapo shilingi milioni 402 zitatumika kupeleka huduma ya nishati ya umeme kwenye kata 10 msalala na kahama mjini huku Milioni 445 zinatumika kwenye mategenezo ya kubadilisha nguzo,vikombe, maboresho ya Transfoma na vifaa vilivyoharibika.

Kata ambazo zinapelekewa huduma hiyo ni pamoja  kata ya Muhungula, Nyakato, Mbulu, Mhongolo, Nyashimbi, Nyihogo sekondari, Kagongwa, Mwendakulima Isaka na Kakola.

Mwisho.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527