MUME AMTAFUNA MKEWE MDOMO NA SIKIO

Mwanamke wa miaka 39 mkaazi wa Tanga Kona, Kenya anauguza majeraha baaada ya mume wake kumnyofoa mdomo na sikio kufuatia ugomvi baina yao.

Jackline Kerubo, mama wa watoto sita, alisema alitaka kwenda kuchuma mboga katika shamba la jirani yake lakini mume wake alimkataza.

Kerubo ambaye ni mume wake aliyefunga naye ndoa miaka 21 iliyopita, anasema kwa sasa anahofia maisha yake pamoja na watoto wake.

Alisema jirani yake aliingilia kati baada ya mume wake kuapa kumpa fundisho . Hata hivyo baada ya kipigo hicho Mume wake alitoweka nyumbani.

Akizungumza na waandishi wa habari, alisema mume wake alitenda unyama huo akiwa jikoni kwa kumpiga kichwani na baadae kumtafuna mdomo na sikio.

Mkuu wa Polisi Maryline Oundo aliwaomba wanandoa kutafuta ushauri wanapokuwa na mizozo na kuitaka jamii kutoa taarifa za kesi zinazokiuka haki za binadamu ili kupata msaada sambamba na watuhumiwa kuchukuliwa hatua.

Bi Kerubo kwa sasa anapatiwa hifadhi katika kituo cha polisi Nambale wakati maafisa polisi tayari wameanza kazi ya kumtafuta mtuhumiwa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527