WAKIMBIZI 66,148 WARUDISHWA NCHINI KWAO


Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Masauni amesema wakimbizi 66, 148 kutoka nchi mbalimbali wamerejeshwa katika nchi zao kati ya mwaka 2017 na Aprili 2019, wakiwemo 31,643 wa Burundi.

Kauli hiyo imetolewa leo na Masauni, Bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la  mbunge wa Viti maalum (CUF), Rukia Kassim Ahmed aliyetaka kujua ni lini Serikali ya Tanzania itawarejesha nyumbani wakimbizi waliojaa katika magereza mbalimbali nchini.

Masauni amesema Mkoa wa Kigoma ndio una magereza zenye idadi kubwa ya wakimbizi, “Wapo 91 na kati yao wafungwa ni 38 na mahabusu 53. Wakimbizi ambao wamefungwa gerezani wanarejeshwa katika nchi zao za asili baada ya kumaliza kutumikia vifungo vyao.”


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527