KUTANA NA MWANAMKE BINGWA WA KUUNDA MAJENEZA...MSHAHARA WAKE ZAIDI YA MSOMI WA CHUO KIKUU


 Mama mmoja mjini Nakuru  nchini Kenya amepata umaarufu kutokana na ustadi wake katika kutengeneza majeneza. 

Loyce Atieno aliwacha kazi ya kuuza mboga mwaka wa 2012 na kuingilia kazi hiyo ambayo kwa sasa anaienzi sana. 

Atieno anasema kuwa hajutii hatua yake kwani kwa sasa hutengeneza KSh 45000 kila mwezi pesa ambazo hangepata iwapo angeendelea kuwakatia wakazi wa Nakuru mboga. 
Loyce Atieno akiwa mahali pake pa kazi. 
Si kawaida kwa wanawake kuingilia kazi ya kuunda jeneza nchini Kenya. 
Kisa cha Atieno ni cha kipekee kwani biashara ya jeneza huonekana ya kuogofya ikizingatiwa ni mwiko kwa jamii nyingi nchini Kenya kufikiria biashara inayohusiana na mauti.

 Biashara hiyo huachiwa wachache tu katika jamii na watu hao huwa wanatengwa kwa njia moja ama nyingine. 

"Kuuza mboga hakukuwa kunanipa hela za kutosha kukithi mahitaji ya familia. Niliamua kuiacha na kuingilia utengenezaji wa jeneza ingawa sikumwarifu yeyote. Nilimwambia tu bwanangu nikiwa tayari nimeanza," alisema Atieno. 

Loyce Atieno hutengeneza shilingi 1500 kwa siku katika biashara yake ya kutengeneza majeneza.

Kulingana na Atieno, gharama ya na faida hutegemea muundo wa jeneza huku la wastani akiliuza kwa KSh 30, 000. Ustadi wake katika kupaka na kurembesha jeneza humtenganisha fundi huyu ambaye aliachia masomo yake kidato cha nane lakini kwa sasa anapata takriban KSh 45000 kila mwezi. 

Hicho ni kipato ambacho hata baadhi ya waliosoma hata hadi mpaka chuo kikuu hawakikaribii. 
Chanzo - Tuko

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post