ALIYEKUWA WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA ATOA NENO BAADA YA KUTUMBULIWA


Aliyekuwa Waziri wa Viwanda na Biashara, Joseph Kakunda amesema alitarajia Rais John Magufuli kumuondoa katika wizara hiyo.

Amesema alilitarajia hilo kutokana na mazingira yaliyokuwa jana katika mkutano kati ya Rais John Magufuli na wawakilishi wa wafanyabiashara kutoka Wilaya zote nchini Tanzania uliofanyika Ikulu, Dar es Salaam.

Leo, Rais Magufuli amefanya mabadiliko  madogo katika baraza la mawaziri kwa kutengua uteuzi wa Kakunda na kumteua aliyekuwa naibu Waziri wa Kilimo, Innocent Bashungwa kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara.

Amesema kwa jinsi wafanyabiashara walivyotoa malalamiko yao Ikulu na kuinyooshea kidole Wizara ya Viwanda wakidai haiwatendei haki, kama kiongozi ilipaswa kujiuzulu.

Kakunda ambaye leo Jumamosi Juni 8, 2019 ametimiza siku 210 tangu alipoteuliwa kuongoza Wizara hiyo akichukua nafasi ya Charles Mwijage ambaye pia aliondolewa.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527