UHARIBIFU WA MAZINGIRA WAISHUSHA TANZANIA HADI NAFASI YA 8 VIVUTIO VYA DUNIA


Waziri wa Malisili na Utalii Dk. Hamisi Kigwangala amesema Tanzania imeshuka kutoka nafasi ya pili mpaka ya nane katika vivutio vya dunia sababu akizitaja ni uharibifu wa mazingira.

Ameeleza hayo leo Jumanne Mei 21 bungeni wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Vunjo James Mbatia (NCCR Mageuzi).

Katika swali lake Mbatia amedai kwamba mwaka 1984 Tanzania ilikuwa inashika nafasi ya pili katika vivutio vinavyochea utalii pamoja na miundombinu.

Mbunge huyo amehoji Je kwa sasa Tanzania inashika nafasi ya ngapi na miundombinu inayochochea inashika nafasi ya ngapi?

Akijibu swali hilo Kingwangala amesema utafiti unaonesha kwamba Tanzania imeshuka katika vivutio  kutoka  nafasi ya pili mpaka ya nane sababu kubwa ni uharibifu wa mazingira.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post