MAZOEZI YA KUTUNISHA MISULI YANAATHIRI UWEZO WA KUZAA KWA WANAUME

Wanasayansi wamegundua kuwa baadhi ya wanaume hupunguza uwezo wao wa kupata watoto kutokana na jitihada zao za kutengeneza miili ya kuvutia .

Mazoezi ya kutunisha misuli au kutumia dawa za kuzuia kupata upara zinaweza kuharibu mfumo wa uzazi.

Athari hiyo imetajwa mara baada ya wanasayansi kufafanua madhara hayo.

Wataalamu wanasema kwamba mwanaume anayetumia dawa au anayefanya mazoezi ya kutunisha misuli anaweza kuwa anapata maumivu ya kichwa wakati wa tendo la ndoa na mbegu zake kushindwa kuwa na uwezo wa kuzalisha.

"Nimegundua kuwa baadhi ya wanaume ambao wanakuja kwa ajili ya vipimo miili yao huwa ni mikubwa," alisema Dkt James Mossman, kutoka chuo cha Brown kilichopo Marekani.

Daktari huyo ameiambia BBC kuwa : "Wanaume wanajaribu kutaka kuwa na muonekano mkubwa, huku wanajisababishia madhara ya afya ya uzazi"

"Licha ya kuwa wanajitengeneza wenyewe maumbile yasiyokuwa na uhalisia, lakini wanashindwa kuelewa kuwa wanajiondolea uwezo wao wa kuwa na mbegu za kuzalisha."Dkt. Mossman na Prof Pacey

Miongoni mwa madhara yanayowapata ni homoni zao kushindwa kufanya tendo la kujamiiana kiufasaha kutokana na mazoea yao ya kutengeneza muonekano wa miili yao kuwa chanzo.

Profesa Allan Pacey kutoka chuo chaSheffield ameongeza : " Inashangaza kuona wanaume wanaenda kwenye mazoezi ili kuwa na muonekano mzuri, na mara nyingi lengo ni kuwavutia wanawake na bila kuelewa kuwa wanapunguza uwezo wao wa kuzaa."

Hata hivyo watafiti wanasema kwamba dhana inayofanana na hiyo ya wanaume kutumia dawa ili kutengeneza maumbile yao ina madhara yanayofanana.
Dawa ambazo zinatengeneza maumbile yao na kuzuia nywele zote husababisha madhara katika mfumo wa wa uzazi.

Prof. Pacey aliiambia BBC kuwa : "Ninaweza kusema kuwa kuna wanaume wengi zaidi ya unavyofikiria ambao wanaweza kupata madhara , inaweza kuwa asilimia 90 hivi.

"Mazoezi hayo yanaweza kuongeza tatizo linalofanana kuendelea."

Dkt Mossman amedai kuwa dawa hizo zinaweza kukufanya kuwa na muonekano mzuri wa kuvutia lakini ikakusababishia madhara katika uzazi.

Aliongeza kwamba anadhani kuwa kuna baadhi ambao wanahisi kwamba wanawavutia jinsia nyingine huku wanauwa uwezo wao wa kuzalisha.

Ujumbe mkubwa hapa ni idadi ya vijana wadogo kuwa wahanga wa kuzalisha bado changamoto.
Chanzo - BBC

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527