MBUNGE WA NSIMBO ATISHIA KUVUA NGUO BUNGENI KISA MAJI


Mbunge wa Nsimbo, Richard Mbogo (CCM), ametishia kuvua nguo bungeni ikibidi ili yapatikane maji safi na salama kwenye jimbo lake.


Mbogo ametishia hivyo wakati akichangia mjadala wa Wizara ya Maji bungeni leo Mei 3, ambapo amesema suala la maji halina mbadala hivyo Serikali itatue tatizo hilo jimboni mwake.

Amesema kama ilivyokuwa kwa mtumishi wa Mungu, Ibrahimu, alikuwa tayari kumchinja mwanawe, lakini baadaye Mungu alimpatia mwanakondoo wa kuchinja, mwanawe akanusurika.

“Mheshimiwa mwenyekiti, suala la maji safi na salama si la mzaha, ikibidi niko tayari kuvua nguo hapa bungeni ili nipate suluhisho la upatikanaji wa maji Nsimbo.

“Kama kuonyesha niko ‘serious’ kwa jambo hili niko tayari kufanya lolote, kama kuna jambo mnaweza kufanya mtuambie tufanye, tozo hii ya Sh. 50 ni muhimu sana,” amesema Mbogo.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527