WAZIRI MKUU: KESHO NI SIKU YA MAPUMZIKO


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema kesho tarehe 26 Aprili, 2019 ni siku ya mapumziko na hakutakuwa na shamrashamra za sherehe.

Akizungumza ofisini kwake jijini Dodoma leo (Alhamisi, Aprili 25, 2019), Waziri Mkuu amesema kesho ni siku ya mapumziko kitaifa kuadhimisha kumbukumbu ya miaka 55 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar lakini hakutakuwa na sherehe.

Amesema jumla ya sh. milioni 988.9 ambazo zilikuwa zimepangwa kwa ajili ya sherehe hizo, zimeokolewa na zitapangiwa shughuli nyingine.

(mwisho)

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527