SIDO YAWATAKA WANANCHI DODOMA KUSHIRIKI KATIKA MAFUNZO YA UTENGEZAJI WA BIDHAA ZA NGOZI

Na.Faustine Gimu Galafoni ,Dodoma.
Wananchi mkoani Dodoma wameaswa kutumia fursa za ndani ikiwa ni pamoja na kushiriki katika mafunzo ya utengenezaji wa bidhaa za ngozi ili kufikia Tanzania ya viwanda.



Wito huo umetolewa na Kaimu meneja wa Shirika la kuhudumia viwanda Vidogo SIDO Mkoa wa Dodoma Stephano Martin Ndunguru wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake,ambapo amesema wananchi waache kuwakimbia wageni wanaohamia jijini Dodoma na wao kwenda mbali na mji bali watumie fursa za ndani kuingiza kipato ambacho kitakidhi mahitaji.

Aidha amesema kuwa wananchi wanatakiwa kuwasiliana na SIDO ili kuwa mshirika wa karibu na kujua fursa mbalimbali zinazo tolewa na shirika hilo, huku akiwataka wananchi kushiriki katika mafunzo ya usindikaji wa mazao mbalimbali ili kufikia Tanzania ya viwanda.

Mbali na hilo amesema kuwa bidhaa inayotengenezwa na ngozi ni imara katika matumizi sababu imetengenezwa na wataalamu ambao wamepata mafunzo bora huku wengine wakiwa wamejiajiri kutengeneza bidhaa hizo.

Hata hivyo ndunguru amesema kuwa SIDO wapo tayari kutoa huduma muhimu kwa watengenezaji wa mifuko mubadala ya Rambo kwa kutoa mafunzo,fedha, na kutafuta masoko kwa wakati.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post