WAZIRI WA MAMBO YA NJE AWATAKA WATU WANAOISEMA VIBAYA TANZANIA KUKAA KIMYA SASA


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi, amewataka watu wanaoisema vibaya Tanzania kukaa kimya kwa sasa.

Profesa Kabudi amesema hayo leo Jumatatu Februari 4, Ikulu jijini Dar es Salaam baada ya kuapishwa kuwa waziri wa wizara hiyo na Rais John Magufuli aliyemteua juzi baada ya kufanya mabadiliko madogo ya mawaziri.

“Jana haikuwa siku nzuri kwangu niliamshwa na watu wengine kuambiwa kwamba nimeteliuwa katika nafasi hii, lakini nashukuru kwa kunipa nafasi.

“Huu si wakati wa kuisema nchi yetu, kuibeza na kuipagaza… nchi yetu ilijengwa na mwasisi Mwalimu Julius Nyerere, yeyote Mtanzania mwenye tatizo na nchi hii atutendee jambo moja tu, akae kimya.

“Tuna jambo moja tu kubwa la kujenga mahusiano na wale wanaoitakia mema nchi yetu,” amesema Profesa Kabudi.

Pamoja na Profesa Kabudi, pia Waziri wa Katiba na Sheria, Dk. Augustine Mahiga aliapishwa na baadhi ya Makamishna wa Jeshi la Polisi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527