MWANAMKE APATA UGONJWA WA AJABU WA "KUTOSIKIA SAUTI ZA WANAUME TU"



Mwanamke mmoja nchini China amegundulika kuwa na ugonjwa wa ajabu, ambao huripotiwa mara chache sana kwa watu.

Mwanamke huyo ambaye amejulikana kwa jina la Chen, aliamka na kujikuta hawezi kusikia sauti ya mpenzi wake, na kuamua kwenda Hospitali.

Alipofanyiwa vipimo na madaktari, mwanamke huyo aligundulika kuwa na tatizo hilo, ambapo yeye husikia sauti zote kasoro za wanaume tu pekee.

Tatizo hilo linajulikana kwa jina la 'reverse-slope hearing loss', ambao humfanya mtu kusikia sauti zenye 'mawimbi mazito' pekee. Ugonjwa huo hutokea nadra sana, ambapo imetajwa kuwa kati ya watu 13,000, mtu mmoja tu ndiye anayeweza kuwa na hatari ya kukubwa na ugonjwa huo.

Ugonjwa huo unaweza kusababishwa na vinasaba ambapo pia mtu anaweza akawa hajawahi kusikia sauti ya chini mfano ile ya muungurumo wa friji, na asigundue tofauti.

Kwenye kesi ya bi Chen, imegundulika kuwa alikuwa akifanya kazi kupitiliza, na kuufanya mwili wake kuchoka, kukosa usingizi na kumfanya apate msongo wa mawazo uliompeleka kupata tatizo hilo la kusikia sauti za wanawake pekee.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527