RAIS MAGUFULI ATOA NDEGE KUSAFIRISHA WANAOTAKA KWENDA KUMZIKA RUGE

Rais John Magufuli ametoa ndege ya Serikali kwa ajili ya kuusafirisha mwili wa marehemu Ruge Mutahaba utakaopelekwa Bukoba kwa ajili ya kuzika.

Msemaji wa Familia ya Mutahaba, Raymond Kashasha amesema hayo leo Ijumaa, Machi 1,2019 alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari.

Ruge anatarajiwa kuzikwa kijijini kwao Kiziru wilayani Bukoba mkoani Kagera na atasafirishwa kutokea Dar es Salaam siku ya Jumapili, Machi 3,2019.

Pia ametoa ndege ya Air Tanzania kwa ajili ya watu wanaotaka kwenda kumzika Ruge ambayo itaondoka Dar es Salaam siku ya Jumatatu, Februari 4 asubuhi kwa gharama ya Sh 600,000 kwenda na kurudi.

Na  Hellen Hartley, Mwananchi
ANGALIA VIDEO HAPA

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527