BABA MZAZI WA MMLIKI WA BLOGU YA FULLSHANGWE AZIKWA MKOANI SONGWE


Baadhi ya wanakijiji pamoja na viongozi mbalimbali wakiwa wamebeba jeneza la Marehemu Marehemu Angolwisye Mwambande Bukuku(101) tayari wakiupeleka kwenye makazi ya milele.
John Bukuku ambaye ni Mmiliki wa Blogu ya Fullshangwe ,Baba mzazi wake Marehemu Angolwisye Mwambande Bukuku(101), aliyefariki usiku wa kuamkia , Machi 24, 2019.
Jana alihifadhiwa katika nyumba ya milele katika kijiji cha Iwezi,wilayani Mbozi Mkoa wa Songwe ambapo viongozi mbalimbali walihudhuria mazishi hayo wakiwemo viongozi wa CCM mkoa wa Songwe pamoja na mkoa wa Mbeya.
Marehemu Angolwisye Mwambande Bukuku amefariki akiwa na umri wa miaka 101
John Bukuku ambaye ni Mmiliki wa Blogu ya Fullshangwe akiwa na baadhi ya ndugu zake baada ya kumaliza shughuri za kumzika ,Baba yake mzazi Marehemu Angolwisye Mwambande Bukuku(101), aliyefariki , Machi 24, 2019. na kuzikwa jana Machi 26 katika kijiji cha Iwezi,wilayani Mbozi Mkoa wa Songwe ambapo viongozi mbalimbali walihudhuria mazishi hayo wakiwemo viongozi wa CCM mkoa wa Songwe pamoja na mkoa wa Mbeya.

Bwana alitoa na sasa ametwaa, jina lake lihimidiwe.

Ameen.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527