SUMAYE : UAMUZI WA LOWASSA KUREJEA CCM HAUNIPI SHIDA...KAMA KAAMUA ACHA AENDE

Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Pwani, Frederick Sumaye amesema uamuzi uliochukuliwa na Edward Lowassa kurejea Chama cha Mapinduzi (CCM) hauwezi kumshtua.

Sumaye ambaye pia ni Waziri Mkuu mstaafu akizungumza na Mwananchi leo Ijumaa Machi 1, 2019 muda mfupi baada ya Lowassa kuchukua uamuzi huo amesema, “Mimi haunipi shida, mtu akiamua kuhama chama na kwenda kingine ni uamuzi wake.”

Akijibu swali la Mwananchi kama naye ni miongoni mwa watakaorejea, Sumaye amesema, “Kama kaamua acha aende, sisi tutaendelea kujenga chama na hicho unachokisema cha kuhama ni ndoto ambayo haipo.”

Lowassa aliyetangaza kuhama CCM Juni 28 mwaka 2015 baada ya kueleza kutoridhika na mchakato wa kumpata mgombea urais ndani ya chama hicho, leo Ijumaa ametangaza kurejea CCM na kupokelewa na Mwenyekiti wa chama hicho tawala nchini Tanzania, Rais John Magufuli.

Na  Ibrahim Yamola, Mwananchi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527