CHADEMA YAFUNGUKA LOWASSA KUREJEA CCM..."YEYE NI MTU MZIMA ANAJUA ANACHOKIFANYA"


Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) nchini Tanzania kimesema kuondoka kwa mwanachama wake, Edward Lowassa na kurejea Chama cha Mapinduzi (CCM) hakutakuwa na madhara yoyote.


Hayo yamesemwa leo Ijumaa Machi 1, 2019 na Katibu Mkuu wa chama hicho kikuu cha upinzani Tanzania, Dk Vicent Mashinji alipozungumza na Mwananchi muda mfupi baada ya Lowassa ambaye ni waziri mkuu wa zamani kutangaza uamuzi huo. 

“Tunamtakia maisha mema huko aendapo yeye ni mtu mzima anajua anachokifanya,” amesema Dk Mashinji.

Alipoulizwa iwapo uamuzi wa Lowassa unaweza kukitetelesha chama hicho kikuu cha upinzani Dk Mashinji amejibu kwa kifupi “It will never happen (haiwezi kutokea)”.

Na  Tausi Mbowe, Mwananchi



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527