TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA 12.02.2019 SALAH KUHAMIA JUVENTUS

Juventus wanajipanga kutoa kitita cha pauni milioni 175 ili kumsajili mshambuliaji wa Liverpool na timu ya taifa ya Misri Mohamed Salah, 26. (Sky Arabia)

Mustakabali wa Maurizio Sarri kama kocha wa Chelsea utaamuliwa ndani ya wiki mbili zijazo. (Telegraph)

Wachezaji wa Chelsea walifanya kikao maalum cha kurekebishana katika uwanja wao wa mazoezi wa Cobham jana Jumatatu kufuatia kipigo walichopata cha 6-0 dhidi ya Manchester City. (Mail)

Kocha wa Derby Frank Lampard amepuuzia uvumi kuwa huenda akarithi mikoba ya Maurizio Sarri endapo Chelsea itaamua kumfukuza. (Evening Standard)

Beki wa Tottenham Juan Foyth, 21, amefichua kuwa alikataa kujiunga na klabu ya Paris Saint-Germain ili ajiunge na Spurs mwaka 2017. (Goal)

Barcelona wamefikia makubaliano na klabu ya Eintracht Frankfurt kumsajili mshambuliaji wao raia wa Serbia Luka Jovic, 21, mwishoni mwa msimu. (Diario Sport)

Mshambuliaji wa Juventus raia wa Argentina Paulo Dybala, 25, anakaribia kufikia makubaliano ya kuhamia Real Madrid mwishoni mwa msimu. (AS)

Kiungo wa Paris Saint-Germain Adrien Rabiot, 23, amekuwa akihusishwa na klabu kadhaa na sasa Man United wameingia kwenye mbio za kumsajili

Manchester United wameingia kwenye kinyang'anyiro cha kumsajili kiungo wa Paris Saint-Germain Adrien Rabiot, 23,mwishoni mwa msimu. (AS - via Mirror)

Chanzo:Bbc

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527