KAZI YA SARRI MATATANI DARAJANI

Maurizio Sarri alikuwa katika filamu ambayo watazamaji wa Chelsea hawajaiona , na kitendo cha mwisho hakikuisha vizuri kwa mkufunzi huyo wa Chelsea katika uwanja wa Stamford Bridge.

Sarri alikuwa kama mtu aliyekuwa anawindwa sawa na watangulizi wake kama vile Felipe Scholari na Adre Villas Boas alipokabiliwa na kichapo cha sita bila mbele ya mikono ya Manchester City - ikiwa ni kipigo kikali tangu Chelsea iliposhindwa 7 mtungi na klabu ya Nottingham Forest mnamo mwezi Aprili 1991.

Alikiri kuwa kazi yake huwa hatarini kila mara huku akisisitiza kuwa hajui iwapo yuko hatarini kwa sasa.

Klabu hiyo ya Sarri imefungwa magoli 10 bila jibu katika kipindi cha mechi mbili za ugenini, baada ya kupoteza 4-0 dhidi ya Bournemouth mnamo tarehe 30.

Chelsea iliojulikana kuwa na safu kali ya ulinzi ilifungwa magoli 4 katika kipindi cha pili dhidi ya kikosi cha Eddie Howe katika kipindi cha dakika 25 za kwanza.

Kufikia sasa wameshuka hadi nafasi ya sita katka ligi ya Uingereza wakiwa nyuma ya Manchester United kwa pointi moja ambayo iko katika nafasi ya nne baada ya kuwa mbele ya mabingwa hao wa zamani kwa pointi 11 wakati Mourinho alipoondoka mwezi Disemba.

Chanzo:Bbc

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527