GHARAMA ZA MATIBABU YA RUGE ZAFIKIA MILIONI 650...KILA SIKU ANATUMIA MIL 5 HADI 6

Gharama za matibabu ya Mkurugenzi wa Vipindi wa Clouds TV na Redio, Ruge Mutahaba zimeelezwa kufikia zaidi ya Sh650 milioni hadi sasa huku kila siku akitumia kati ya Sh5 hadi Sh6 milioni.

Kwa muda sasa Ruge yupo nchini Afrika Kusini kwa matibabu ya figo na imeelezwa na mdogo wake, Mbaki Mutahaba kuwa kaka yake anaendelea vizuri.

Mbaki amesema mpaka sasa, Ruge ametumia kati ya Sh500 hadi Sh650 milioni kwa matibabu hayo na zaidi ya Sh530 milioni zimetolewa na Clouds Media.

Amesema gharama za matibabu ni kubwa lakini aliwashukuru watu mbalimbali wanaoendelea kujitolea kwa namna moja au nyingine.

Na Hellen Hartley, Mwananchi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527