JAMAA AMUUA MCHEPUKO WA MKEWE BAADA YA KUWANASA WAKIFANYA MAPENZI KITANDANI KWAKE


Jamaa mmoja mwenyeji wa eneo la Bandari, Kisumu nchini Kenya anasakwa na maafisa wa polisi kwa tuhuma ya kumuua mchepuko wa mkewe baada ya kuwanasa 'live' wakihondomola tendo la ndoa 'wakifanya mapenzi' kwenye kitanda chake.


Majirani wameeleza kuwa jamaa huyo ambaye ni Mwendesha boda boda alirudi nyumbani kutoka kwa mkewe mwingine usiku wa manane Februari 7,2019 na baada ya kuingia ndani alishangaa kuona simu asiyoijua pamoja na nguo zikiwa kwenye kiti.

Alichukua mwendesha bodaboda huyo baada ya  kuona vitu hivyo aliingia moja kwa moja hadi chumba cha kulalia ili kushuhudia ni nini kilichokuwa kikiendelea. 

Alikasirika baada ya kumuona jamaa huyo/mgoni akimmchovya mkewe kitandani akachukua kisu na kumdunga mara kadhaa na kumuua papo hapo.

"Alinaswa akiwa uchi, nguo zilikuwa kwenye kiti na simu yake ilikuwa mezani. Mumewe aliingia chumbani na kumpata mume huyo amemlalia mkewe. Mlango haukuwa umefungwa,’’ jirani moja alisimulia.

Hata hivyo, mkewe huyo aliweza kuponyoka akiwa uchi na kujinusuru ili kuepusha balaa zaidi kutokana na fumanizi hilo. 

Inadaiwa kuwa muuaji huyo alichukua nafasi na kusafisha kisu chake kwa kutumia chupi ya jamaa huyo pole pole kabla ya kutoroka.

 Polisi walifika eneo hilo na kuchukua mwili wa marehemu huku msako ukianzishwa kumkamata mume huyo muuaji.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527