WANACCM KAGERA WACHANGIA UJENZI WA DARASA LA SEKONDARI


Mjumbe wa Halmshauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Kagera, Ramadan Kambuga (aliyevaa shati ya rangi ya njano) akiwaongoza makada wenzake wa chama hicho katika ujenzi wa chumba cha darasa katika Sekondari ya Kalema Kata Buendangabo ikiwa ni utekelezaji wa ilani ya CCM.
Bw. Ramadan Kambuga akipanda mti katika eneo la shule hiyo.

Bw. Ramadan Kambuga, akiwa na makada wenzake wakati wa ujenzi wa darasa hilo. 

Wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa Kushirikiana na viongozi wa chama hicho ngazi ya Wilaya Bukoba mjini mkoani Kagera wameshiriki zoezi la usombaji mawe kwa ajili ya ujenzi wa chumba cha darasa katika Shule ya Sekondari ya Kalema Kata Buendangabo na kupanda miti ikiwa ni kuazimisha miaka 42 ya
kuzaliwa kwa chama hicho. 

Mjumbe wa Halmashauri Kuu wa chama hicho Mkoa wa Kagera, Ramadan Kambuga ambaye pia ameshiriki zoezi hilo,amesema kuwa ujenzi wa chumba hicho cha darasa ni utekelezaji wa ilani ya CCM. 

Kutokana na msongamano wa manafunzi darasani katika shule hiyo Bwana Kambuga ametoa kiasi cha shilingi laki moja ili isaidie kuongeza nguvu na kuweza kuondoa adha hiyo ambayo inawakabili wanafunzi wa shule hiyo. 

Bwana Kambuga pia amesema wao kama wadau wa maendeleo na wasimamizi wa serikali kupitia Chama cha Mapinduzi wataendelea kuunga mkono jitihada zinazofanywa na serikali  ili kuwaletea maendeleo wananchi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527